.

Tamani Mafanikio, Gusa Jamii Kubwa


Na: MROPE Wa MROPE
 Tufanye mambo yote tufanyayo lakini tukumbuke mwisho wa siku tunawajibika mbele za Mungu ambaye ndiye muumba wetu. Kwa mantiki hiyo basi ni vyema tunapotafuta mafanikio tusitafute mafanikio ili "kuwashushua" wakina fulani au ili kujionesha na kupata sababu ya kujisifu ati sisi ni bora sana kuliko wengine. Ninajua kwa yakini kila mtu anapotafuta mafanikio anasukumwa na
jambo fulani moyoni mwake lakini msukumo wowote wenye dhamiri ovu ni ngumu kufanikiwa au mafanikio hayo humuondolea mtu amani ya moyo.
Aidha siri kuu ya mafanikio ni dhamiri ya kuwafikia watu wengi bila kuwabagua kwa namna yoyote maana kila mmoja yupo namna alivyo kwa makusudi maalumu hivyo kutafuta mafanikio ili kumnanga fulani au ili uonekane bora ni janga la safari ya mafanikio yako.
Mara nyingi nimekuwa nikitoa mfano wa Mfalme Suleimani (Solomoni) ambapo alipotokewa na Mungu na kuulizwa amtendee nini? Yeye alijibu kwa unyenyekevu, "Naomba hekima ya kuongoza watu ulionipa". Wangapi leo wangejibu hivyo? Wengi wangesema, "Unajua Mungu hawa watu ulionipa ni wengi tena ukikutana nao wanapenda sana kuombaomba nami sina pesa kwa hiyo nijaze miutajiri".
Mafanikio yoyote yana siri kubwa na Mungu huwa anamuinua mtu ili kuinua wengine wakiwepo wale ambao hawakupendi na wanakuchukia kwa bidii sana. Yusufu alipata kuwa waziri kwa mfalme ili awasaidie chakula nduguze (wakiwepo wale waliomuuza) wakati ule wa njaa.
Kwa hiyo ikiwa mtu yoyote ana dhamira na mafanikio makubwa lazima awe na dhamiri moyoni kwamba akifanikiwa ataitazamaje jamii yake.
Kila mmoja wetu anajijua siku ya kufanikiwa kwake atatazama vipi wale "aliowafunika". Kuna wengne hawaioni kabisa jamii kwa mema au mabaya ila wanajiona wao tu katika ulimwengu wao wa ubinafsi.
Mungu humpa vingi mmoja ili kufikisha wengi ili nao wakifanikiwa wajifunze kwa mfano huo lakini kujiona peke yako ndiko kunazuia mafanikio ya wengi.
Tukumbuke kabla ya kufikiwa mafanikio yetu dhamiri zetu hujaribiwa na Mungu na hata wale wa mlango wa nyuma hujaribiwa pia kwa kutakiwa kushirikisha damu za wawapendao kuwa kinywaji cha mapepo.
Mafanikio yoyote yadumuyo ni yale yanayogusa maisha ya wengine pia na sio kuwatesa au kuwadhihaki.
ALOYCE MROPE, Che Mrope Wa Mrope (fb) Mbeba Maono (fb page) 0787641417/0766656626/0715366010
Previous
Next Post »