Na: MROPE wa MROPE- Iringa
Kila binadamu chini ya jua ana uhuru wa
kuchagua; kufanikiwa au kutofanikiwa. Mafanikio
hayamfuati mtu shida tumezaliwa nazo maana sote tulizaliwa tukiwa watupu
na mengine yote tuliyonayo yawe mazuri au mabaya tumeyapata tukiwa hapa
duniani. Uamuzi wa
kufanikiwa au kutofanikiwa upo
katika matendo yetu ambayo ni mazao ya fikra na matamshi yetu. Hakuna
binadamu ambaye hana matendo, kila sekunde tunatenda jambo fulani la
lazima au si la lazima, baya au zuri.
Haikwepeki lazima
kila binadamu atende; atake au asitake. Mafanikio yetu au kushndwa kwetu
kupo katika matendo hayo maana kila sekunde mtu hufikiri, hutazama,
husikiliza, hutembea, huongea, n.k.
Katika matendo hayo
ndiposa mtu hutenda kwa faida au kwa hasara, hujenga au hubomoa,
hufikiri kulaani au kubariki, hutazama matambiko au mbinu za mafanikio,
husikiliza mema au maovu n.k. Katika uchaguzi wa nini tutende na nini
tusitende ndipo ilipo njiapanda ya kushinda na kushindwa.
Kwa
namna hii imekupasa kujiuliza katika matendo yako unayotenda mangapi
yanakuinua na mangapi yanakushusha? Mangapi unatenda kwa ajili ya kesho
yako na mangapi unatenda kwa ajili ya kesho ya wengine huku ukiamini
unaitendea haki kesho yako? Ukitafakari vizuri utagundua wapo watu
wanamaliza hata wiki nzima hawajatenda matendo yanayojenga kesho yao ili
kuibomoa au kuisusa.
Jiulize pale unapobishana kwa
jazba kuhusu nani mkali kati ya Mesi na Ronaldo, Man Pacquiao na
Mayweather, Ali Kiba na Diamond n.k unakuwa umeijenga kesho yako kwa
namna gani? Jiulize unapolalamika kutaka uonewe huruma unakuwa umeijenga
kesho yako kwa mtindo gani? Kuna wakati watu wamekuwa mashabiki wa
mambo yasiyowahusu toka mwanzo mpaka mwisho wa wiki, Januari mpaka
Desemba bila hata wao wenyewe kujijua.
Fikiri upya kuhusu matendo yako.
ALOYCE MROPE, Che Mrope Wa Mrope (fb), Mbeba Maono (fb page) 0787641417/0766656626/0715366010
Sign up here with your email