.

Huwa Natenganisha Kati Ya Mtu Kumiliki Vyeti Na Mtu Kuwa Na Akili


Na: Albert Sanga, Iringa. 

Mtu anaponiambia kuwa huyu mtu ni msomi ama hiki kitu kimefanyika kisomi huwa sitishiki wala kubabaika. Huwa natenganisha kati ya mtu kumiliki vyeti na mtu kuwa na akili. Ukibahatika kuwa navyo vyote viwili basi una bahati lakini wasomi wengi wanaishia kuwa na vyeti pekee; akili eidha hawana
ama huamua kutozitumia.

Wanaweza kukueleza jambo hadi ukasema, heeee! ila wao watakwambia wanachokuambia ni "cha kisomi". Wana matatizo kila kona ila kwenye biashara ndio utachoka! Kwanza wasomi wengi wa biashara na uchumi "hawanaga" hata biashara walau za genge tu, hawana! Ila wakute wakikuelezea biashara "kisomi" utapenda! Waambie wakafanye, watakupiga chenga. 


Kuna wasomi nilikutana nao 2012 pale Ilula wakaniambia wamefanya utafiti wa kilimo cha nyanya na wamegundua kuwa biashara hiyo haina faida hata tone kwa namna wakulima wanavyolima pale Ilula. 

Kwanza nikashangaa, nikawaeleza, "mnasema hakuna faida, mbona hizi nyumba na maendeleo yote Ilula ni matokeo ya nyanya, kivipi hazina faida?" Wakanitolea magraph yao meeeengi, wakanipa sijui nini nini sample za waliowahoji; yote wakitaka kunidhihirishia kuwa walichonieleza kipo kisomi!


 Mi nikawaambia labda mngeniambia wakulima wanapata faida pungufu ya inayotakiwa lakini kusema kilimo hiki hakina faida kabisa, nakataa! Nikaachana nao maana niliona wamenizengua tu. Msimu uliofuata nikafanya biashara ile ya nyanya nikapata faida kubwa sana tofauti na walichosema. 


Hawa wasomi kwenye biashara waonage hivi hivi, wana vimambo vyao vya kiutafiti ambavyo ukisema uvizingatie vinaweza kugeuka miluzi ya kukupoteza ~SmartMind~


Top of Form

Bottom of Form


Previous
Next Post »