.

Kila Binadamu Ana Utu wa Ndani Na Utu Wa Nje ( Shetani Ana Maslahi Na Umaskini)


Na: MROPE wa MROPE
NDANI YA KILA MTU UNAYEMFAHAMU KUNA MTU MWINGINE USIYEMFAHAMU:
Kila binadamu ana utu wa nje na utu wa ndani. Utu wa nje unaweza kuwa imara kuliko utu wa ndani na utu wa ndani unaweza kuwa imara kuliko utu wa nje.
Vyovyote iwavyo hatima ya maisha ya mtu huamuriwa na
utu wa ndani. Huko ndiko mtu hufanya tafakari na kuchukua maamuzi ya mwisho. Maana yake ni kuwa utu wa ndani ukiwa mlegevu hata maamuzi ya mtu yatakuwa malegevu na matokeo atakayopata mtu huyo ni malegevu pia.
Kuna wengine unaweza kuona ni jitu lenye afya njema na nguvu nyingi lakini utu wake wa ndani ukawa dhaifu sana na hapo ndipo utasikia, "huyu mambo yake hayaendani kabisa na jinsi alivyo".
Kuna mwingine ana afya njema na ni pandikizi la mtu na utu wa ndani ni imara basi watu watamsifu kwa kusema, "vile unavyomuona na ndivyo alivyo mpaka 'rohoni'". 
Wengine wana miili midogo wanafanya mambo makubwa, wengine umri mkubwa wanafanya mambo ya umri mdogo kabisa, kwa hiyo ni wazi kila binadamu ana mtu wa pili ndanimwe ambaye anaathiri fikra, matamshi, na matendo na hatimaye matokeo ya maisha yake. Katika hali halisi ni nadra sana utu wa nje kuwa bora kama utu wa ndani ni wa ovyo ovyo. Wengine utu wa ndani ni ovyo lakini kwa nje utu wake ni bora, huyo si bora bali anapretend (kujishaua).
Kwa hiyo jukumu la mtu kufanikiwa lazima lianze kujengwa kwa mtu wa ndani yako. Ukiwa imara ndani hata kama nje watakudharau wala hutatishika. Huwezi kusimamia maamuzi mazito ambayo jamii inayaona kinyume na ukabaki imara kuendea malengo yako kama utu wa ndani ni legelege.
Malengo yote ya mafanikio kwanza yanapata upinzani katika ulimwengu wa roho toka kwa shetani na wajumbe wake maana mafanikio yako yanakuondoa katika uwezekano mkubwa wa kunasa katka mitego yake mingi anayoitumia kupitia umaskini.
Kuna vibaka, majambazi, makahaba, machokoraa, ndoa zinazobomoka kupitia umaskini na kwa namna hiyo shetani ana maslahi na umaskini na Mungu hajatuwekea fungu la kushindwa wala umaskini ili kutuepusha na hayo.
Umaskini sio mpango wa Mungu. Kwa hiyo mafanikio yako yanapngwa na shetani na kisha binadamu wasiokutakia mema na ndiposa unapaswa kuwa imara katika utu wa ndani ili usimame imara kuelekea maamuzi yako na kama haupo imara ndani utapga mbwembwe na mayowe bila kufanikiwa.
Nini kifanyike? 1. Jiimarishe katika imani ya kushinda 2.  Jifunze kufikiri, kutamka na kutenda katika kushinda 3. Fanya mafanikio unayoyatarajia kuwa sehemu ya ukombozi wa wale wanaoteswa na kukosa mafanikio kama yale utakayoyapata wewe. Imarisha utu wa ndani kisha uyaendee mafanikio yako. Che Mrope Wa Mrope, Mbeba Maono (fb page), 0766656626/0715366010/0787641417

 
Previous
Next Post »