Na: Meshack Maganga--Iringa,Go Big or Go Home
“Watu wangu
wanaangamizwa kwa kukosa maarifa” ni moja ya mistari maarufu sana katika kitabu
kitakatifu Biblia. Ni moja ya sentensi zinazoigusa jamii yetu kwa sasa, hapa
Tanzania, Afika na dunia kwa ujumla. Kitabu hiki cha ‘Graduate with PlanB in Mind’ kimekuja wakati muafaka kabisa kwa
Taifa letu na dunia kwa ujumla. Hii ni kwa sababu
kimetokea wakati ambao vijana
wengi wa kike na wa kiume waliopo katika
ngazi mbalimbali za kielimu wamekuwa wakiyumba yumba sana na wasijue cha
kufanya wanapokuwa wamehitimu masomo yao. Wengi wao wamekuwa ni wahitimu
walalamishi badala ya kuwa wahitimu wafumbuzi wa matatizo ya kijamii
inayowazunguka.
Nilipokisoma
kitabu hiki kilipokuwa katika hatua za awali, mawazo yangu ya kina yalilipuka
upya. Nilitamani kama ningekisoma kitabu hiki mwanzo kabisa nikiwa shule ya
sekondari ya kawaida. Nilishasoma vitabu vingi sana vilivyoandikwa kwa Lugha ya
Kiswahili, na kingereza vikiongelea namna ya kufanikiwa katika maisha, namna ya
kushinda kwenye usaili, na vingine vingi vya aina hiyo. Lakini sikuwahi kusoma
kitabu ambacho kingenipatia mbadala wa maisha. (Plan B).
Wengi wetu tunapotoka
vyuo vikuu tunakuwa tumebeba wazo moja kuu la ‘ajira’, kana kwamba ajira ni
moja ya amri kumi takatifu za nabii Musa ambazo ukiikosea moja tu unapigwa
mawe. Tunapofika mitaani kwetu tunakuta
kitu kingine. Tunapokuwa chuo kikuu ama katika ngazi za chini za elimu
tunajisahau sana. Tunakuwa kwenye ulimwengu wa chuo kikuu kana kwamba hatutaondoka
kwenye majengo ya vyuo na kutufanya tusahau ulimwengu wa halisi wa mtaani
kwetu.
Kama wewe ni
mwanafunzi wa ngazi yoyote ile unayoifahamu, hakikisha unakisoma kitabu hiki, kwanini uendelee kuangamizwa kwa kukosa maarifa na kuendelea kuamini mawazo ya walioshindwa ama kubebwa na matukio
ya mitaani ama kwenye mitandao ya kijamii? Ama mawazo ya wanafunzi wenzako na
mawazo ya walimu na wazazi waoishi maisha ya uoga? Wanaoamini kwamba maisha ni
ajira pekee? Tumekuwa watu wenye kubebwa
na wazo moja tu la ajira kana kwamba bila ajira maisha hayaendi.
Tumechelewa
sana kuangalia na kujifunza kwa wenzetu wa nchi za dunia ya kwanza ambako
maisha ni zaidi ya ajira. Tupo kwenye dunia ambayo wasomi na wajasiriamali
wanatakiwa kuwa wabunifu wabuni ajira,maana kila anaehitimu akiwaza kuajiliwa
basi kuna hatari ya kuwa wategemezi kwenye vipengele mbalimbali vya maisha. Bahati
nzuri Tanzania ni moja ya nchi pekee duniani iliyosheheni fursa za kila aina
fursa unazoweza kuzifanya hata kabla ya kutoka shule ama chuo. Uamuzi unabakia
mkononi mwako, kujifunza maarifa na kuzitumia fursa ama kutojifunza ili
ukihitimu masomo yako ubakie kuwa mlalamikaji.
Mawazo yaliyo
andikwa na Mwandishi wa kitabu hiki ni mawazo yaliyofanyiwa utafiti wa kina na
lengo lake ni kuzalisha mitazamo mipya miongoni wa wasomi waliopo vyuoni,
wazazi, walimu, viongozi mbalimbali wa kisiasa, kidini na kijamii kwa ujumla.
Ninatoa rai yangu kwa wazazi, walimu na wakuu wa vyuo na shule kukinunua kitabu
hiki na kukiweka kwenye maktaba zao ili kiwe msaada kwa wanafunzi na watoto
wao.
Dunia ya sasa ni dunia ya wanadamu wanaojua ni kitu gani wanaweza.Siyo
dunia ya kufuata mkumbo wala bendera kufuata upepo na matukio ya kijamii kama
ilivyokuwa katika karne ya zama za kati za mawe, enzi ambazo wanajamii walikuwa
wakifanya mambo kwa kubanwa na mazingira ya wakati huo. Kauli za ‘Kupata ni
majaliwa’ Ng’ombe wa maskini hazai’ serkali haituthamini’, ‘sijasoma’, mimi ni
mlalahoi ama mlalatabani, 'mkoa wangu ni wa pembezoni,’ ‘kabila letu
limesahaulika’, nk, ni kauli za kimaskini, ni kauli za kutafuta
visingizio. Kwakukisoma kitabu hiki
utatambua nguvu ya mawazo yako ya kina na utatambua kusudi la wewe kuwepo
duniani. Pigania kile ukitakacho usivunjwe moyo na waliochoka kiakili,
waliochoka kufikiri, na wasiokuwa na malengo. Na wanaosema ponda mali kufa
kwajwa. Go Big or Go Home.
Meshack C.
Maganga.
Sign up here with your email