KILIMO
CHA MITI KINAVYOZALISHA MAMILIONEA MKOANI IRINGA
Na: Meshack Maganga- (Iringa) Go Big Or Go Home
Makala
hii ni matokeo ya mjadala mkali wa WANAMFANIKIO-GOLD, kundi mahusi lililoanzishwa
na rafiki yangu Makirita Amani. Siku ya tarehe 24.11.2012 baada ya harusi
yangu, nilipigiwa simu na Makirita akiniomba niongoze mjadala wa wanamafanikio
jumapili. Niliona ni bahati ya pekee sana maana duniani tupo Wanadamu bilioni
7, na Tanzania tupo Wanadamu zaidi ya milioni 40 hii ilikuwa bahati na fursa
mojawapo kuwahi kuzipata.
Siku
ya mjadala ilipofika niliulizwa maswali mengi sana, mojawapo ikiwa ni ufafanuzi
na maelezo ya jumla juu ya faida ya kilimo cha
Miti, swali jingine lilikuwa ni changamoto katika
kilimo cha miti na uchumi kwa ujumla, jingine
lilikuwa ni kitu gani kinaweza kusaidia kubadilisha fikra za watanzania kuelewa
faida itokanayo na kilimo cha Miti?
Mwanamafanikio mwingine alitaka kufahamu ni kwanini
ni watanzania wachache sana wanajihusisha
na kilimo cha miti? Na akasema nina ushauri gani kwao na watanufaikaje kiuchumi kupitia kilimo
cha miti?
Nitajibu
maswali haya kwa ujumla wake hapa chini. Kwanza: Kilimo
hiki cha miti ni (SOMA ZAIDI)
uwekezaji wa muda wa kati na mrefu (middle& long term
investments). Kiutamaduni watanzania wengi huwa hawavutiwi na uwekezaji wa muda
mrefu. Hata hivyo kama una mpango wa kuwa na “financial freedom” usikwepe
kufikiria uwekezaji wa muda mrefu. Waingereza husema “Information is power”.
Wengi hawajachangamkia fursa hii kwa kukosa taarifa tu. Tulipokuwa tunaendelea
na mjadala ule, nikambukumbuka “Mentor” wangu Albert Sanga, aliposema ‘Wengi wa
watanzania wanapenda sana hela za chapchap! Ukitaka umpate mtanzania mpe fursa
inayoonesha kuwa fedha itapatikana kesho, wiki ijayo, mwezi ujao na ikizidi
sana mwaka ujao. Ukitaka mtanzania asiwe rafiki yako, mweleze habari za kufanya
mambo yatakayoleta faida ama fedha kuanzia miaka mitano, kumi, ishirini ama
hamsini mbele. Kwanza hatakuelewa na pili atakupuuza’.
Nilisema kuwa Kilimo cha miti ya mbao, nguzo za umeme, nguzo
za kujengea, milunda na miti ya kuni na dawa, kimepata umaarufu wa ghafla miaka ya
hivi karibuni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ongezeko la mahitaji ya
mazao ya miti na changamoto ya mazingira. Hapa nchini mkoa wa Iringa ni moja ya
mikoa maarufu inayoongoza kwa misitu mikubwa
iliyopandwa na watu binafsi, mashirika ya kigeni na serkali. Miti
inatumika kwa mbao, nguzo za umeme, nguzo za kujengea pamoja na utengenezeaji
wa karatasi na madawa. Hivi sasa kumeibuka fursa nyingine mpya ambapo mashirika
ya kimazingira kutoka Magharibi yananunua hewa ya ukaa. Kwa maana hiyo unaweza
kupanda shamba la miti halafu ukawa unakusanya dola kwa kuuza hewa ukaa wakati
ukisubiri miti ikomae uvune mbao, nguzo ama miti ghafi ya kutengenezea
karatasi. Hii ni sawa na kutengeneza pesa ukiwa umelala nyumbani kwako (Making money while sleeping- UNAWEZA
KUCHAGUA KUAMINI AMA KUTOAMINI), vile vile unaweza kufuga nyuki na kuendelea
kuvuna asali.
Kilimo cha miti, kina faida sana, pengine
baadhi ya watanzania wa ndani na nje ya nchi wengi wao hawajabahatika kusikia
faida ya kilimo hiki, ama wengi wao wamekisikia na kuzifahamu faida za kilimo
cha miti. Wanashindwa waanzie wapi, na ndio maana mpaka sasa wanaolima miti ni
watanzania wachache sana, na wale waliojitokeza kulima miti ndio mamilionea wa
miaka michache ijayo, Hii ni
kwasababu, ukipanda ekari moja ya miti ya mbao ambayo ni jumla ya miti mia sita
hadi miatano, ikishakomaa unaweza kuuza mti mmoja kwa bei rejareja shilingi
elfu 25 kwa kadilio la chini kabisa, kwa hiyo 25,000 x miti labda mia 5 ni sawa
na milioni 12,kwa bei ya sasa. Je miaka 8 ijayo itakuwa shilingi ngapi? Ndio
maana pale Mafinga na vijiji vyake, vijana wadogo waliojiingiza kwenye kilimo
cha miti ni mamilionea wa miaka ijayo. Na wewe msomaji unanafasi ya kuwa milionea
kama utachagua...!
Baadhi ya
changamoto nilizo kutana na nazo tangu nilipoanza kilimo cha miti; nikukosa pesa za kutosha hasa kipindi cha
kupanda miche mipya kinapoaanza, maana unapopanda miti mpya unatakiwa uwe na
pesa ya kutosha. Changamoto nyingine ni tatizo la usafiri, mashamba mengi ya
miti yapo nje ya mji wa Iringa, unatakiwa usafiri kilomita nyingi kwa siku
mpaka kufika sehemu yalipo mashamba hasa katika wilaya ya Mufindi na Kilolo.
Tulijadilina mambo mengi sana siku ile ya mjadala, msomaji unanafasi
ya kuwasiliana na mimi kwa simu ama email ama kupitia mitandao ya kijamii. Na Kabla
sijahitimisha makala hii ninapenda
kulisema jambo lifuatalo,kauli za ‘ Kupata ni majaliwa’ Ng’ombe wa maskini
hazai’ serkali haituthamini’, ‘sijasoma’, mimi ni mlalaohoi/ mlalatabani’ nk,
ni kauli za kimaskini, ni kauli za kutafuta visingizio. Tumia vizuri mawazo
yako ya kina ufanikiwe. Jielimishe, soma vitabu vingi, vya mafanikio. Tembelea
maduka ya vitabu. Kuna duka moja kubwa sana la vitabu pale Dar, linaitwa ‘The
House Of Wisdom’ ukifika pale hata kama usiponunua kitabu, lakini ukisoma
vichwa vya vitabu vile, lazima utoke na kitu kitakachobadili maisha yako.
Achana na mawazo yatakayo kukatisha
tamaa, achana na marafiki wanaokupotezea
muda wako, walalamishi, jenga urafiki na waliofanikiwa. Ni mpango wa Mungu ni
kukuona wewe ukishi maisha ya furaha,
maisha ya utele na mafanikio katika Nyanja zote za kiuchumi na kijamii na
kiroho. Kama kuna kitu kinaitwa bahati, basi asilimia 90 inakwenda kwa wale
watafutaji na wachapakazi na wasiokata tamaa. Ninawatakia mafanikio mema. BINADAMU
WENYE MAFANIKIO HAWACHOKI KUTAFUTA- Go Big or Go Home email meshackmaganga@gmail.com
https://www.facebook.com/Fresh-Farms-Trading
Sign up here with your email