.

Unaweza Kujiona Mjanja Sasa lakini Muda Si Mrefu Unaweza Ukaumbuka.


 Na: Albert Sanga--Iringa

Yesu Kristo alisema, "Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake, na mengine yote mtazidishiwa". "Pattern" (sio context) ya falsafa hiyo inaweza kuwa "applied" kwenye uchumi, kwamba, "Tafuteni uwekezaji kwanza na vitega uchumi na kisha hayo mambo yanayohitaji matumizi mtazidishiwa". 

Unajua ni kwa nini watu wengi wanafeli kiuchumi?
Ni kwa sababu wakipata fedha jambo la kwanza wanafikiria matumizi badala ya uwekezaji na vitega uchumi. Wanakimbilia kununua mavazi, kujenga nyumba za kuishi, kununua magari ya kutembelea, kumiliki simu za gharama, starehe, n.k. 

Mwanzo hufurahi lakini muda si mwingi baadae wanagota. Lakini ukipata fedha, (iwe ni mkopo, iwe umepewa, iwe ni umejiwekea akiba, iwe ni mshahara n.k), ukianza kwa kuhangaikia uwekezaji na vitega uchumi basi uwe na uhakika kwamba mengine yote, (kama magari ya kutembelea, nyumba za kuishi, mavazi makali n.k) utazidishiwa.

 Unapowekeza, mwanzoni unaweza kuonekana kama unaechelewa ama ukachukuliwa poa ama ukaonekana hauendi na wakati; lakini utakapoanza kuvuna uwekezaji wako; kila mtu lazima atakupa saluti! Ukianza kwa kutumia usithubutu kujilinganisha wala kucheza karibu na mtu alieanza kwa kuwekeza, unaweza kujiona mjaja sasa lakini muda si mrefu unaweza ukaumbuka. ~SmartMind~











Meshack Maganga---Go Big Or Go Home
Previous
Next Post »