.

Usifikiri Kuzaliwa Mwafrika Ni Tatizo...?










By Elizabeth Samoja

Baada ya kuwaona waafrica tukiwanyenyekea sana watu wa ngozi nyeupe nilikuwa nikidhani wao kunavitu vya ziada mungu kawapendelea...baada ya kukua,kusoma elimu ya darasani,na baadae kuwekeza muda wa kutosha kusoma vitabu vya mafanikio na biblia nikagundua kuwa wanadamu wote ni sawa Tatizo la mwafrica kunakitu hajakigundua ndo maana anaendelea kuwa alivyo leo...

Watu wote ni
sawa,watu wote wanatabia zinafanana..majungu,wizi,ulevi,roho mbaya,roho nzuri,kupenda anasa,etc...vithibitisho..Biblia hebu soma tabia ambazo zinakemewa ndani ya kitabu kitatifu....tabia mbaya zote zimekemewa...Je kitabu hicho kiliandikwa na mwafrica???? hicho ni kithibitisho number moja......

Number mbili toka nimeanza kusoma vitabu vya success kunatabia waandishi wanazikemea kama chanzo cha kufanya watu wasisonge mbele ikiwa ni uvivu,kutokujiamini,kutojiandaa,kutokupa elimu ya kina juu ya jambo unalotaka kulifanya na mengine mengi...vitabu hivyo vingi vimeandikwa na mzungu kwa kuangalia mazingira yanayowazunguka.....lakini ukweli waafrica katika hili nalo hawapo nyuma...wamejaa hofu,hawathubutu chochote,hawako tayari kujifunza,wanachukulia mazungumzo ya vijiweni na kukomalia utafikiri yanatokana na utafit etc....

Kunakitu ambacho mungu alificha maarifa yote ndani yake na ambao tu wataweza kupangundua ndo wataifurahia dunia hii,lasivyo wengi tutakuwa tumekuja duniani kusindikiza maisha....na wenzetu wajanja walijaribu kukifanyia utafiti na kukipata huku wakimwomba roho mtakatifu awaongoze nacho ni POWER OF SUBCONSCIOUS MIND .....hapa ndo panapoleta tofauti.....usipoirisha vizuri hii sehemu ya ubungo wako....kwisha habari....shetani nae analijua hili...ndo maana kawakamata watu katika eneo hili pia.......Waafrica wengi wanaamini katika uchawi na kwamba nguvu za kiza ndo kila kitu....yupo kazini na hirizi,anaenda kanisani na hirizi,kila mwisho wa mwaka anamwaga damu makaburini na kuomba mizimu kinyume na mpango wa mungu...kwa kufanya hivi na kuendeleza haya yote vizazi na vizazi mfumo mzima wa subconscious mind unaharibika na kuamini mambo yasiyo ya msingi na kuuwa uwezo wake wa kukuwezesha kufikia mambo ambayo mungu alikuumba kuja kuyafanya hapa duniani......

Sisemi kwamba ngozi nyeupe hawapo wanaoamini katika uchawi.ila africa imekuwa kero kiasi kwamba mtu hafikirii chochote..kila gumu akikutana nalo anahisi uchawi.....pia hajafunguka upande wa pili wa jinsi ya kuimentor subsconcious mind yake......kitu chochote ukikirudia zaidi ya mara 21 moja subconscious mind inajua ni kweli...ukirudia kusema uongo fulani zaidi ya mara 21 unaifanya system yako kuamini hivyo,ukienda kwa waganga kila unapokutana na tatizo subsconscious yako inaamini uganga ni kila kitu........hivyo kuuwa uwezo wako wa kufikiri kinyume na hapo

Mungu si mganga wa jadi...ila wengi wanataka awe mganga wa jadi....ndo maana kanisa litakalotangaza miujiza ya kumiliki nyumba na gari kwa muda mfupi litapata waumini wengi haraka sana....kwasababu watu hawa bado nguvu za giza zimewakamata na kuamini katika mafanikiko ya haraharaka kupitia mtumishi huyo mganga wa jadi aliyekuja kwa njia ya kujifanya ni mtumishi wa mungu........

Sasa nini kilichotofautisha mwafrica na mzungu?.....Kabla sijaongelea itambulike kuwa hata wazungu si kama tunavyowafikiria....kuma pareto rule inasema hivi 80/20 kwa maana hiyo mafanikio makubwa tunayoyaona kwa wazungu yameletwa na asilimia 20% ya wazungu....wengine ni followers tu.....sasa kama ndo hivyo....asilimia 20% africa nayo ikichukua jukumu hili tutafika mbali sana sana...si lazima kila mtanzania ama mwafrica alete mabadilikoa africa...wachache wenye fursa zao wangezitumia vizuri kama wenzetu walivyofanya tungefika mbali sana na pasingekuwa na mwafrica kumuona mzungu kama mungu....bali wangekuwa watu tu kama sisi.....mfano kunavyuo vingi tunakimbilia kusoma huko nje vilianzishwa na watu binafsi kama sehemu ya kupunguza mapungu yaliyo katika mfumo mama...kwani sisi tunashindwa nini??? Ubinafsi au? kila mtu anajiwazia yeye na watoto wake tu au?....

Shetani anakiri sana anajua fika juu ya kazi ya sadaka na kila roho inayopokea sadaka inafanya kazi sawa sawa.....mfano ukitoa sadaka kwa mganga wa kienyeji yale mapepo yanaletwa maishani mwako na kuongoza maisha yako na yana nguvu kweli na utaona mafanikio uliyoyaomba....sema shetani alivyokuwa mjanja zaidi hakuweka shariti gumu sana mfano fungu la kumi ambalo limeonekana kuwa tatizo kwa wengi.....mtu anayeingiza mil 100 ukimwambia atoe 10% anaona du 10mil zote ziende church si mtumishi atanenepa sana....ila mganga yeye hanahaja ya 10% ukimpa tu hata mil moja na ng;ombe unaendelea kubalikiwa.......hahahahhaha...

lakini pia shetani akawa mjanja zaidi...anakupa na matokeo moja kwa moja ili akukamate ipasavyo.....Lakini ukweli ni kwamba ukielewa aina za sadaka,kazi za kila sadaka na mashariti yake kwa upande wa mungu hakuna linaloshindikana...biblia inamifano mingi ya watu waatiifu ambao mumgu aliwainua sana sana...........Shetani bado mjanja tu...hata akupe mali lazima mwisho wa siku akuaibishe tu.....na mara nyingi mali zake huondoka na aliyezizalisha na anamashariti ya kijinga sana kukupima kama wewe unaakri timamu au la.....mfano anakwambia nitakupa kila ktu ila ulale chini,usivae viatu,ulale na mama yako,ulale na dada yako etc...hapa anakupima tu....Mungu wetu hanamasharti ya kijinga maana anajua mtu aliyemuumba ni wa thanmani sana na anatakiwa kufurahia utajri wake akiutengeneza kwa njia nzuri

Ukilijua neno litakuweka huru na hapatakuwa na haja ya kumnyenyekea mzungu,mzungu anatakiwa kuwa partner tu na si kwamba yeye ndo kila kitu....Kunakazi ya ziada inahitajika kufanyika africa ili kumkomboa mwafrica kifkra...
Wazee wetu kama akina mandela,nyerere walitumia muda wao hapa duniani kuhakikisha sisi ngozi nyeusi nao tunaoneka huru na kutambulika duniani...sasa tunahitaji akina nyerere wengine na si lazima wawe wanasiasa ambao wamepata fursa ya kulijua hili nao waweze kuplay their part.....tusiendelee kunyamaza,tuendelee kupambana kumkomboa mwafrica katika ukoloni mamboleo...

Kwa kuwa sasa kila kitu kipo wazi wazi sababu ya globalization tuwasome wenzetu,tujipange wakija kushituka wanakuta hatuhitaji mikopo yao na misaada yao ambayo inaendelea kutufanya watumwa kwao.....hivi tuchukulie wewe ni mzazi halafu bado unamuhudumia kijana wako mwenye miaka 50 kama mtoto hii ni kweli jamani? Tuzindukeni.....unajua kwanini mandela alifanikiwa? alienda england kusoma law na akawa mwafrica kwa kwanza kuanzisha law firm....katika masono hayo yalimwezesho kugundua kitu cha oppression ndo akaja akaanza mapambano....unatakiwa kumjua adui wako kwa kina then unaandaa mkakati wa kupambana nae.........Mungu ibariki Africa,Mungu Ibariki Tanzania.....bado tunahitaji ukombozi,na ukombozi huu utaletwa na sisi wenyewe,hao wazungu usidhani wanapenda ukombozi wetu kiuchumi...wao wanapenda madini yetu,gesi zetu n.k kwa sababu wameshatusoma wakatuona hola...na wao hawaandani madhara ya miaka 3-5 wao wanaandaa madhara ya miaka 50 hadi mia.....so mwanzoni mwa msaada utanona raha ila mwishowe ni machungu...................

Wako katika ujenzi wa taifa la leo na la kesho
Elizabeth Samoja





Meshack Maganga---Go Big Or Go Home
Previous
Next Post »