Na: Meshack Maganga, Iringa MERO investment GO
BIG
Sasa hivi kutokana na ugumu wa masharti
yanayowezesha watu kupata mahitaji kwa mikopo au njia nyingine, kuna idadi
kubwa ya watu ambao wameamua kuazisha biashara kwa kushirikiana. Pengine
wengine wamelazimishwa na ushindani uliopo kufanya biashara kama timu kuliko
mtu mmoja mmoja.Lakini kama wasemavyo wataalamu wa mafanikio, mtu mmojammoja
huwa anajikiza mwenyewe wakati mwingine.
Kama ni hivyo,watu wanapo kuwa zaidi ya mmoja,
hata wawili, ni suala lisiloweza kuepukwa. Hii haina maana
kwamba, ushirika wa kibiashara ni mbaya, hapana. Bali suala ni kwamba uangalifu
ni muhimu sana.
Ndoa inaweza kulinganishwa na mtu na mshirika
wake kibiashara, kwa sababu ya kufanana mambo mengi, kati ya ndoa na
ushirikiano wa kibiashara. “Hadi kifo kije kitutenganishe” hiki ni
kibwagizo cha kawaida kusemwa mbele ya kasisi kama kiapo kwa mke au mume
mtarajiwa. Lakini ukifanya hivyo kwa mshirika wako kibiashara utakuwa hujaona
mbali tena ni jambo la hatari sana.
Hicho tu ndicho kipengele ambacho ndoa na
ushirikiano kibiashara vinatofautiana. Lakini maeneo mengine yote ni kama
sawa.Ndoa imara na bora ni ile ambayo wahusika walijuana vema na kupanga mambo
yote muhimu mapema. Walikubaliana au kupingana kuhusa watoto, kazi, wazazi na
ndugu, imani na mengine. Walitafuta ufumbuzi wa kila kikwanzo cha baadaye
kwanza.
Mara nyingi watu wanaoanzisha biashara ya (SOMA ZAIDI
kushirikiana (partnership) huruka hatua moja muhimu sana: kuweka makubaliano
kwa maandishi chini ya mwanasheria. Hata Kama utafanikiwa kuanzisha biashara
nzuri na yenye mafanikio na mshiriki wako wa kibiashara, je, una mawazo kwamba
mtakuwa pamoja katika biashara hiyo katika maisha yenu yote?
Biashara ambazo hazijitenganishi na wamiliki
usalama wake ni mdogo, ukuaji wake ni wa kusuasua na urefu wa uhai wake daima
huwa mashakani. Ingawa mimi nilikuja kugundua kuwa ‘kumbe’ nilifisika kwa
sababu ya biashara zangu kukosa mfumo rasmi wa kiutawala, baadae nilipata funzo
kubwa sana kuhusu hatua za uanzishaji na uendeshaji wa biashara katika mfumo wa
kikampuni.
Wajasiriamali wanapofikia uamuzi wa kuanzisha
kampuni (partnership) kuna hatua chache tu za kufuata. Kwanza wanatakiwa
kuandaa nyaraka za kampuni, ambazo zinaeleza muundo na mfumo wa kampuni
inayokusudiwa. Nayaraka hizi zinajulikana Kama, ‘Article of Association’
inaelezea muundo wa ndani wa kampuni wakati nyaraka nyingine ni ‘Memorundum of
Association’ hii ikiwa inaeleza uwezo na mipaka itakayokuwa nayo kampuni
inayokwenda kuundwa.
Hebu fikiria,umefikia umri wa miaka 90-bado
kweli utakuwa una uwezo wa kuchapa kazi katika ushirikiano
huo? Utafika muda,mtalazimika kuvunja ushirikiano wenu bila kujali kwamba
mnapata faida au hasara. Kwa kuzingatia hili, anza ushirikiano na mshiriki wa
kibiashara wako mkiwa na malengo. Mkifanya hivi pale pale mnapoanza ushirikiano
wenu, mtavuna matunda yaliyo bora sana kwenye ushirikiano huo.
Kufanya biashara na mshiriki wa kibiashara ni
sawa na janga linalosubiriwa kutokea. Olabisi na Saley walikuwa madaktari, kila
mmoja alikuwa akifanya kazi yake Tanzania. Waliamua kwenda kuazisha hospital
Namibia.Walipomuona mwanasheria kwa ushauri, aliwaambia wafanye makubaliano
kimaandishi.
Katika kuandika makubaliano, Olabisi
alipinga mambo ambayo Saley alikuwa anataka yawemo katika mkataba huo. Baada ya
miezi miwili ya majadiliano ya mkataba ule, Olabisi alitoka kwenye chumba
cha mwanasheria kwa hasira kutokana na kikao kuwa cha moto.Sasa huu ni mvutano
uliotokea hata kabla ya ushirikiano wenyewe haujaanza.
Je,wangekuwa wameshaanza ingekuwa rahisi kwa
tatizo hili kutafuti waufumbuzi? Olabisi na Saley hawa kuongea tena
ingawa walikuwa katika fani moja. Usije ukadhani kwa sababu tu, lengo letu ni
kufanya shughuli fulani, kila kitu mnakubaliana. Ni vema, yote yakawekwa wazi,
Hata yale yanayoonekana madogo kabisa. Watu wanaojiingiza katika ushirika wa
kibiashara huku wakiwa na malengo ya muda mrefu ambayo ni malengo tofauti
kabisa. Tengenezeni malengo ya muda ya mrefu kwanza, na yale ya muda mfupi
yatokane na yale ya muda mrefu.
Peterson na Chrislouw walianzisha Kampuni yao
wakiwa na kila mmoja hisa sawa na mwingine, yaani 50 kwa 50. Hii ina maana ya
watu walio sawa, yaani kwa umiliki wa kampuni yao. Walianza biashara yao bila
malengo yoyote,yaani kama walikuwa wanabahatisha ilikuwa ni aina ya upotezaji
muda.
Mambo yakageuka na biashara yao kuwa kubwa na
yenye mafanikio makubwa. Biashara yao ilivyozidi kuwa kubwa ndivyo uadui kati
yao ulivyozidi kuwa wazi. Kuna wakati fedha inaweza kuwa ndiyo kigezo cha hisia
zetu –ikiwa nyingi tunakuwa wakorofi, ikiwa kidogo tunakuwa wapole,au kinyume
chake.
Ilitokea siku moja Peterson akilalama kwamba
Chrislouw anatamaa na anenda kinyume na malengo yetu ya zamani kwamba
tutawajali wateja wetu kwa kuzalisha bidhaa bora na kwamba Sasa hivi kitu
muhimu kwake ni kutaka kuwa rais wa kampuni hii kubwa na kupata mamilioni ya
fedha.
Peterson kwa upande wake, hakutaka kufanya kazi
kwa bidii wala kuhitaji kuwa tajiri mkubwa. Alikuwa akihitaji kile ambacho
kingeweza kuihudumia familia yake. Chrislouw kwa upande mwingine alikuwa
ameachana na mkewe akiwa na watoto kadhaa –kazi yake ilikuwa ndio maisha yake.
Chrislouw alilalamika; Peterson anairudisha
kampuni hii nyuma.Hufanya kazi kwa lengo la kuikuza kibiashara. Palepale mwanzo
yangejitokeza haya yanayojitokeza sasa wakati wanajadili malengo ya muda mrefu.
Kila mtu angekuwa ameonesha wazi ni kitu gani kinamvuta katika kuingia katika
ushirikiano huo.
Kuondoa tofauti hizi kubwa walitakiwa wakati
wanafanya makubaliano kuweka vipengele ambavyo vingemfanya Chrislouw aweze
kununua hisa za Peterson Au makubaliano hayo yangekuwa yameainisha kwamba
mshiriki wa kibiashara wa tatu angeruhusiwa kuingizwa ili kumpunguzia mzigo
Chrislouw wateja wateja wanapo kuwa wengi.
Lakini badala ya makubaliano kuwa 50/50
yangebadilishwa na kuwa labda sitini kwa arobaini ili kufidia kazi nyingi
ambazo Chrislouw anafanya zaidi kuliko Peterson. Muda muafaka wa kuyaweka hayo
yote ilikuwa ni pale mwanzoni wakati bado walikuwa na maelewano ya kirafiki,
siyo ya kibiashara.
Ingawa mijadala ya kutengeneza makubaliano
inakuwa na misuguano mikubwa, baada majadiliano, ushirikiano wenu utakuwa
katika msingi imara.Badala ya kupotaza muda mwingi kwa ajili ya kutatua
matatizo yatokanayo na kutofanya mabadiliko mapema, muda huo utakuwa ukitumika
kwa ajili ya tija.
Biashara yeyote inaratibiwa na mazingira
mbalimbali ya kisheria. Moja wapo ni kutakiwa kupafanya mahali pa kazi kuwa
salama kwa wafanyakazi pamoja na kuwalipa stahili zao kwa wakati. Biashara
yeyote ukiona haithamini wafanyakazi, watendaji ama vibarua wake basi uwe na
uhakika kuwa anguko lake lipo karibu.
Tofauti na kwenye siasa ambako kipimo cha uzuri
wa chama cha siasa ni wakati wa uchaguzi; kwenye biashara alama ya kwanza ya
biashara ama kampuni kupoteza dira ni kukimbiwa na wafanyakazi, kupungua kwa
wateja na kushuka kwa mauzo. Katika eneo hili kuna jingine ambalo ni kutoa
bidhaa na huduma salama.
Nilieleza
kwa kina baadhi ya mambo ya muhimu yanayopaswa kuzingatia kabla na wakati wa
kuanzisha biashara za ushirikiano (kampuni, patnashipu n.k). Wasomaji wengi
wamewasiliana nami wakinipongeza na kutoa maoni yanayopanua mjadala huu. Leo
ninaendelea na sehemu ya pili ya makala hii katika pembe zingine mtambuka.
Wengi wetu tumesikia watu waliokuwa marafiki
katika biashara wakikorofishana. Kwa sehemu kubwa hii ina tokana na kufanya
mambo kienyeji. Mike ni mmoja wa watu walikumbwa na matatizo kama haya:
‘mshirika wangu katika biashara aliamua kuuza biashara yetu bila ridhaa yangu.
Tulianzisha biashara yetu toka ziro hadi mauzo
kufikia shilingi milioni mia sita Kwa mwaka anasema Mike. Halafu anaendelea,
Nilikuwa ninachapa kazi kama punda na hatukuwahi kugombana. Lakini nyuma ya
pazia, kwa kuwa hisa zake katika biashara zake katika biashara yetu ilikuwa
asilimia 60 akawa amempata mnunuaji na kuamua kuiuza biashara yetu.
Alinilazimisha tuiuze; nilikuwa sina fedha za
kununua hisa zake baada ya kuuzwa marafiki zangu wakaniona nina bahati baada ya
kupata fedha nyingi. Lakini nilikuwa sijali sana kuhusu fedha. Nilimpoteza
rafiki yangu mpendwa na kazi yangu niliyokuwa naipenda sana. Usaliti huu
ulinishitua sana. Masalia ya mshituko huo bado yapo na ndio yanaisha
kidogokidogo.
Yote haya ni matokeo ya kudhani mshirika
wako anafikiri na kuamini katika kile unachoamini. Kuweka mambo wazi na kwa
makubaliano kabla ya biashara ni muhimu sana. Fedha hubadili mitazamo ya watu,
hasa wanaoamini kwamba, fedha ni kila kitu na wale wanao amini kwamba bila
mtaji huwezi kuanza biashara.
Kwanza inabidi kufahamu kuwa hakuna watu
waliozaliwa kuwa marafiki bora ama marafiki wabaya kibiashara. Watu wote
wanatengenezwa kutegemea na mazingira ya kazi. Kwa maana hii si ndugu, mke wako
ama familia yako watakaokuwa wasaidizi bora katika biashara zako.
Isipokuwa unatakiwa kuwa na mbinu sahihi za namna
ya kuwapata watu makini watakaobeba uchungu kama ulionao wewe katika biashara
zako. Kwa maana hii iwe ni watu unaohusiana nao kiundugu ama usiohusiana nao,
wote unatakiwa kuwaajiri ama kufanya nao kazi kwa werevu mwingi.
Suala la kuwapata washirika makini linatakiwa
kuanza na wewe kubaini tabia ama hulka za watu ambao utaendana nao katika
mawazo na maamuzi ya kibiashara. Jambo la pili ni kuangalia matakwa yao ya
ndani (motives) na la mwisho ni uwezo wako wa kuwajengea uwezo wa kufanya kazi
na kukaa nao kwa muda muafaka.
Mjasiriamali maarufu duniani Robert Kiyosaki
ambaye mwaka huu ameibuka kuwa mshindi wa Tuzo ya “12 days of Finance Winner”
katika makala ya "The benefits of being in Rich Dad's Business
Owner Quadrant™ vs. Self Employed Cash flow Quadrant™ " ameeleza
kuwa wakati alipokuwa akifanya biashara kwa kutegemea nguvu zake mwenyewe
na ujanja wake alioupata chuo kwa kupewa kazi binafsi ama za vikundi maarufu
kama (individual assignment or group assignment) na Profesa wake ama
mhadhiri alijua atafanikiwa mapema baadaye kutokana na mabadiliko ya dunia
akagundua kwamba kufanya biashara bila ushirika na wenzako ni sawa na ‘kutaka
kuvuka bahari ya Hindi kwa Mtumbwi uliotoba’
UJASIRIAMALI bila kuwa na mfumo rasmi wa
uendeshaji ninaweza kuufananisha na ile hulka ya ndege aina ya mbuni ya
kujificha mchangani. Mbuni kwa kawaida huwa ana asili ya kuficha kichwa chake
mchangani pindi aonapo hatari ama anapotaka kuwa salama katika eneo lolote
lile”.
Albert anasisitiza kuwa wajasiriamali wanapokuwa
wamesajili rasmi (kampuni) au biashara zao, wanalazimika kuwa na mfumo rasmi wa
kiutawala pamoja na utunzaji wa kumbukumbu za kimahesabu. Kunapokuwepo na
kampuni hailazimiki wamiliki wa kampuni wawepo ili biashara ziende.
Hii ni faida tofauti na ilivyo kwa
wafanyabiashara binafsi (sole proprietor) ambapo wao ni biashara na biashara ni
wao. Wao wakifa na biashara zinawafuata nyuma yao makaburini. Lakini wamiliki
wa kampuni wakifa, ama mmoja wao akifariki kampuni inaendelea kuishi kwa kuwa
yenyewe ni mtu kamili kisheria (legal person) na haki ya kila mmoja itakuwepo
kwasababu kuna Legal Document.
Kwenye makala ya "South
Park's" Investing Lesson: Imeelezwa kwamba,
wenye ndoto ya kuanzisha biashara ya kushirikiana wanatakiwa kuwa na Mpango wa
biashara (Business Plan) Mimi ni mmoja wa wenye ndoto hiyo (partnership).
Mpango biashara, ambao kwa maana ya kawaida
(surface meaning) na maana ambayo mwalimu wangu wa chuo kikuu Dr.Mahali aliwahi
kuiniambia “ni vifaa vya kufanyia uamuzi wa kibiashara”. Kwa kiasi fulani,
muundo na yaliyomo kwenye mpango wa biashara hutokana na malengo ya pamoja ya
washiriki. Ni sharti mpango wa biashara ijumuishe kila habari inayohitajika
kuamua kutekeleza lengo fulani la kibiashara.
Kwa mfano, mpango wa biashara wa shirika lisilo
la kifaida hufafanua ukubalifu kati ya mpango wa biashara na malengo ya shirika
hilo. Kimsingi washiriki wa mtaji hujihusisha na uwekezaji wa awali, uwezekano
wa kufaulu na kutathimini jinsi ya kutamatisha. Mpango wa biashara wa mradi
unaohitaji fedha utahitaji kueleza kwa nini rasilimali zilizopo kwa sasa,
nafasi za biashara zinazoibuka, na faida ya ushindani endelevu itawaletea
ufanisi mwishoni.
Utayarishaji wa mpango wa biashara huhitaji
maarifa kutoka kwa taaluma za biashara mbalimbali: fedha, na usimamizi wa
wafanyakazi, usimamizi wa ujuzi-nafsi, usimamizi wa ugavi, usimamizi wa
shughuli, na masoko, miongoni mwa mengine. Ni jambo muhimu kuangalia mpango wa
biashara kama mkusanyiko wa mipango midogo midogo, moja kwa kila taaluma kuu ya
biashara.
Mpango wa biashara mzuri unaweza kusaidia kufanya
biashara nzuri iwe ya kuaminika, ya kueleweka, na kuvutia kwa mtu ambaye hana
ufahamu wa biashara hiyo. Uandishi mpango mzuri wa biashara haumaanishi kuwa
utafaulu lakini unaweza kusaidia katika kupunguza uwezekano wa kutofanikiwa kwa
biashara ya ushirika.
Nilipotembelea nchi ya Zambia miaka miwili
iliyopita nilibahatika kusoma magazeti na vitabu mbalimbali lakini moja ya
makala ambayo iliniingia kichwani kama mjasiriamali na mpenda biashara ya
ushirikiano, na nimhimu kunukuu katika Somo la
leo ni ile ya Rais wa kampuni ya ‘Colgate’ duniani Ian Cook. Yenye
kichwa kisemacho Kanuni na maadili mema ya Colgate-palmolive.
Ian Cook anasema kuwa Uamuzi wako ni moja wapo ya
mali yako ya thamani sana. Unafaa kuepuka shughuli ama ushirika wowote ambao
unagongana na ama unaonekena kugongana na uwezo wako wa kufanya uamuzi wa
kujitegemea kwa masilahi ya Kampuni. Migongano inaweza kutokana na hali nyingi.
Ni vigumu kuelezea yote hapa, na haitakuwa kila mara rahisi kutofautisha kati
ya shughuli kamili na zisizo kamili.
Katika makala hiyo washirika wa kibiashara
wanasisitizwa kwamba, unapokuwa na hoja amadukuduku, muone meneja wako ama
mshauri wako wa kitengo cha sheria kabla ya kuchukua hatua yoyote. Miongozo
ifuatayo inatumika katika hali ya kawaida ya migongano. Usifanye uwekezaji
wowote unaoweza kuathiri uamuzi wako wa kibiashara.
Sera za Kampuni zinakataza watu wa Colgate
kumiliki hisa ama kuwa na hamu ya kumiliki katika Kampuni inayoshinda na ama
inayofanya biashara na Colgate. Kizuizi hiki hakitumiki kwa kumiliki viwango
vidogo (kwa ujumla chini ya 1%) vya hisa za Kampuni inayouza hisa kwa umma ila
tu uwekezaji huo usiwe wa kiwango kinachoweza kuunda dalili ya mzozo wa
upendeleo..
Kuanza na mwisho ndicho kitu cha msingi katika
biashara ya ushirikiano. Hii hujibu swali; hivi mimi na mshirika wangu wa
kibiashara tunamalengo sawa? Tunajisoma? Tunajifunza mambo mapya kilasiku?
Tunasoma vitabu vya utambuzi na maarifa ya biashara? Mshirika wangu na mawazo
hasi ama chanya?
Anamvuto? Ana dira
ya maisha? Ana aminini katika misemo ya ponda mali kufa kwaja? Maisha
yake ameyaweke rehani kwa wanasiasa? Au ana amini kwamba mkombozi wake ni
serikali au kiongozi wake wa kisiasa? Mkijua kila mmoja ana lengo na nini na
kwanini?,kwa vipi? ni muhimu kuliko kufanya mambo kienyeji ambayo huleta
faida za kienyeji na mwisho wa kienyeji. Kwaleo niishie hapa. Sisi sote ni
washindi-na tunahitaji ushirikiano.
Meshack Maganga---Go Big Or Go Home
Sign up here with your email