.

Hapa Ndipo "Tunapoachana Na Kupotezana" Kiuchumi.


Na : Albert Sanga - Iringa 
Kimsingi kwenye maisha kila mtu, kuanzia watoto mpaka watu wazima fedha hupita mikononi mwao; kinachotofautiana ni viwango. Kwa hiyo, utaona kuwa kupata fedha sio tatizo kwa sababu wengi(kama sio wote) tumewahi ama huwa tunapata fedha. Kazi mbili ngumu linapokuja suala la
fedha ni kutunza na kuziongeza fedha zinazopita kwako ama unazopata. 

Hapa ndipo "tunapoachana na kupotezana" kiuchumi. Hekima inatuambia kwamba fedha yeyote inayopita kwako, (iwe ya kupewa, uwe mshahara, iwe faida, iwe mkopo ama vyovyote) ni lazima uichukulie kama mbegu; kwanza izalishe thamani ndipo itoke, kinyume na hapo fedha haiwezi kuvutiwa kuishi na wewe. ~SmartMind~
Previous
Next Post »