.

2015 KATAA KUKATA TAMAA, Mtu yoyote hawezi kukukatisha taama juu ya jambo lolote bila ridhaa yako




Na: Hadija Jabiri – Iringa 

Wengi tuna hamu kubwa ya kufanikiwa maishani. Kati ya sababu ambazo hutufanya tusifanikiwe ni pamoja na kukata tama tunapokuwa kwenye safari ya
mafanikio. Ili uweze kufanika kwenye maisha katika enoe lolote (biashara, ndoa, dini nk) lazima uwe mtu usiyefahamu maana ya neno kukata tamaa. Mafaniko ni sawa na barabara yenye kona nyinyi, milima na mabonde na si njia nyoofu kama wengi wanavyofikiria.  Ni rahisi sana kwa mtu kuianza safari ya mafanikio lakini wengi huwa tunaishia njiani pale tunapoanza kukutana na changamoto za safari.

Kati ya sababu zinazoweza kumfanya mtu akate tamaa ni pamoja na ushauri, sina maana ya kuwa ni vibaya kupokea ushauri toka kwa watu, lakini kubwa ni kulitafakari kila unaloshauriwa na kuchukua lile unaloona lina msingi kwako, tunapaswa kufunga masikio yetu ili tusisikie kabisa maneno ya kutukatisha tamaa. 

Bila shaka huu ni wakati muafaka kwako kuanza kusema hivi, Kama jambo ninalotaka kulifanya au ninalolifanya lina manufaa kwangu na naamini litakuwa na mafanikio mbeleni, kama jambo hilo halimchukizi mungu na kama jambo hilo halipinzani na sheria za nchi basi nitalifanya na sitasikiliza maneno ya watu wanaojaribu kunikatisha tamaa.

 Tunapaswa kuwa makini sana na aina ya watu tunaowaomba ushauri pale tunapotaka kufanya jambo Fulani au tunapokutana na changamoto kwenye jambo Fulani. Ni vyema sana pale tunapotafuta ushauri juu ya jambo Fulani kuwafata watu waliofanikiwa kwenye jambo hilo.
Sababu nyingine inayokatisha wengi tamaa ni kushindwa, ikiwa kama mtu alijaribu jambo Fulani na akawa na matarajio makubwa ya kufanikiwa basi ikitokea hakufanikiwa kama alivyotarajia hukata tamaa kabisa na hata kiogopa kufanya tena.

 siamini kama kushindwa kunatakiwa kukukatishe tama, kushindwa ni moja kati ya vitu vya msingi unapotaka kufanikiwa, baada ya kushindwa hupaswi kukata tamaa au kuogopa kujaribu tena na badala yake unatakiwa kukaa chini na kujiuliza sababu gani haswa zilipelekea ushindwe kufikia mafanikio na wakati mwingine unapofanya jambo hilo tena basi unalifanya kwa ustadi zaidi. mfano Kama umeweka lengo la kufika Dar es saalam ukitokea Makambako kwa usafiri wa gari moshi na ukaambiwa njia ya gari moshi imeharibika basi panda basi au ndege, mwisho wa siku hakikisha unafika Dar na si kughairisha safari kwasababu tu njia ya gari moshi imeharibika.
Waliofanikiwa wameshindwa mara nyingi sana. 

Thomas Edison aliyegundua taa ya  umeme alifanya majaribio zaidi ya elfu tisa kabla ya kufanikiwa, Donald trumph ambaye nimwekezaji mkubwa kwenye majengo nchini marekani alishafilisika miaka ya tisini lakini hakukata tamaa na sasa ni mmoja kati ya watu wenye nguvu kubwa nchini Marekani. Je Thomas Edson angekata tamaa leo tungekuwa na taa za umeme? Na kama Donald trumph angekata tamaa leo dunia isingeziona Trumph Towers? Hivyo moja kati ya sababu kubwa zinazowatofautisha waliofanikiwa na wasiofanikiwa ni uwezo wa kuinuka baada ya kuanguka. Waliofanikiwa wanatabia ya kuendelea kwenda mbele bila kujali wameanguka mara ngapi wala ubovu wa njia wanayopita.

Kumbuka, Mtu yoyote hawezi kukukatisha taama juu ya jambo lolote bila ridhaa yako. Jiamini na amini unaweza kupata chochote unachokitaka maishani mwako. Tupo mwanzoni kabisa mwa mwaka 2015, fanya uamuzi leo na anza kuzifuata ndoto zako kwa gharama yoyote bila kuwasikiliza wakatisha tamaa.
’’ Your life is your choice’’













Previous
Next Post »